Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Februari 15, 2013

TEKNOHAMA - KOMPYUTA IMEGAWANYIKA KATIKA SEHEMU INAYOSHIKIKA NA SEHEMU ISIYOSHIKIKA!


Photo Credity By: http://metrology.zeiss.com

 Hakika kompyuta ni kifaa kilichoundwa katika utaalam wa hali ya juu. Unapokuwa unaitazama kompyuta, yaani unapokuwa unaiona monitor, keyboard, case na vinginevyo unakuwa unaona sehemu ya ‘nje’ ya kompyuta. Unakuwa unaiona sehemu ijulikanayo kama hardware part. Hardware part ni sehemu ambayo unaweza kuishika na kuiona kwa macho. Ni sehemu ambayo ni hard au ‘ngumu’ kwa maana ya kwamba inaonekana na kuweza kubebwa na kufanyiwa marekebisho. Sehemu hii ya kompyuta haiko peke yake katika ufanyaji kazi wa kompyuta.

Yenyewe kama ilivyo haiwezi kufanya lolote; ni kopo lisilo na maana! Ni kama unaponunua baiskeli na kuiweka ndani. Itakuwa na manufaa kwako endapo tu utaiendesha. Ni kama unapokuwa na gari ambalo bado halina mafuta. Ili liweze kujongea utahitaji kuliwekea mafuta. Vivyo hivyo kompyuta haitaweza ‘kujiendesha’ yenyewe bila kuwa na muendeshaji (ambaye ni wewe). Kompyuta haitaweza kufanya kazi kama itakuwa na hardware part peke yake. Ni lazima kuwe na muendeshaji wa hardware part hiyo.

Sehemu ya kompyuta ambayo ni muhimu sana katika kuifanya ifanye kazi iliyokusudiwa ni ile ‘isiyoonekana’. Ni sehemu ambayo huwezi kuiona na inajulikana kama software part. Tazama jinsi maneno yalivyotumika: hardware na software ambayo yanatia msisitizo katika ‘ugumu’ na ‘ulaini’. Sofware ni mkusanyiko wa maelekezo maalum ambayo kompyuta hupewa ili kuiwezesha kufanya kazi kulingana na maelekezo hayo. Kwa jina jingine software inafahamika kama computer

Ni namna gani software na hardware hufanya kazi kwa ushirikiano?

Kama nilivyosema hapo awali hardware part ya kompyuta ni mkusanyiko wa sakiti mbalimbali ambazo zimeunganishwa katika mfumo maalum unaoiwezesha kompyuta kufanya kazi. Lakini ni lazima sakiti ya kompyuta ipewe maelekezo maalum ili iweze kufanya kazi. Ni kama kuiamuru runinga yako ioneshe kituo Fulani cha matangazo ambacho unataka kutazama. Kwa kutumia dhana hii wataalam wa mambo ya kompyuta waliamua kutumia mkusanyiko wa maelekezo uitwao software ili kufanikisha hili. Software ni mkusanyiko wa maelekezo mbalimbali yaliyogawanyika kulingana na kazi yanayotakiwa kufanya. Kuna maelekezo ya kuwasha kompyuta, kuna maelekezo ya kuizima kompyuta, kuna maelekezo ya kutoa ishara za hatari, maelekezo ya kutoa mlio na kuacha kutoa mlio, maelekezo ya kuandaa picha za video na za kawaida, maelekezo ya kuhifadhi habari zinazoandaliwa na mengine chungu nzima. Hii inamaansiha kuwa kuna software tofauti tofauti kulingana na kazi zinazotakiwa kufanya. Kuna software ya kuandikia, software ya kupigia mziki, software ya kuendeshea mitambo, software ya kutengeneza sauti, softwares za kuendesha mitambo mbalimbali kama robots, ndege, camera za ulinzi nk.

Mkusanyiko wa software mbalimbali hufanya vipi kazi katika hardware?

Software zote huunganishwa na kupangiliwa kufanya kazi kwa kutumia software kuu ijulikanayo kama system software au operating system kwa kifupi OS. OS ni maelekezo mama ambayo huingizwa katika kompyuta mara tu kompyuta inapokuwa imetengenezwa. Ni maelekezo ambayo huiendesha kompyuta katika kupokea na kutoa maelekezo mengine ambayo binadamu hutaka ifanye. OS ndiyo huiwasha kompyuta na kuiweka katika hali tayarifu kwa ajili ya kufanya kazi. Kifuatacho ni sehemu ndogo ya kile ambacho OS hufanya unapotaka kuitumia kompyuta: Unawasha kompyuta kwa kubonyeza kitufe cha kupokea umeme Umeme hutiririka katika sakiti nzima ya kompyuta OS hufahamu kuwa umeme umeingia hivyo huiwasha kompyuta OS hutizama kama kila sehemu muhimu ya kompyuta ipo kwa mfano keyboard, mouse, monitor n.k

Baada ya muda kompyuta inakuwa tayari imewashwa na iko tayari kufanya kazi ikimsubiri mtumiaji ailekeze nini cha kufanya. Mtumiaji wa kompyuta hutumia peripheral devices kama keyboard na mouse katika kuilekeza kompyuta ifanye kile anachokihitaji. Na hao ndipo panakuwa na maelekezo mengine ambayo niliyazungumzia hapo mwanzo. Kwa mfano kama mtumiaji anataka kuandika barua basi itambidi aanzishe maelekezo yatakayomwezesha kuandika barua hiyo. Maelekezo haya madogodogo hutekelezwa na programu ndogo inayfanya kazi pamoja na programu mama ikijulikana kama application software. Kwa maana hii tunaweza kusema kuwa software part ya kompyuta imegewanyika katika sehemu kuu mbili; system software na application software.

Je, maelekezo haya yajulikanavyo Kama application software na system
software hueleweka vipi ndani ya kompyuta?

Kwa hakika unaweza kujiuliza ni vipi maelekezo haya hutambulika na sakiti ndogondogo za kompyuta. Lakini ni dhana rahisi tu kuilewa. Ni kama wewe unapozungumza na mtu ambaye hatumii lugha unayoizungumza. Itakubidi uzungumze na mtu huyo kwa kutumia mfasiri (mkalimani). Vivyo hivyo maelekezo ya kompyuta inabidi yatafsiriwe na kuwekwa katika mfumo ambao hardware ya kompyuta itayaelewa. Lakini jambo moja la kufahamu ni kwamba maelekezo haya huandaliwa au kuandikwa kwa utaalamu maalum ili yaweze kueleweka katika kompyuta.

Utaalam huu hutumiwa na wanasayansi wa kompyuta. Utaalam huu hufahamika kama programming. Utaalamu huu hutumia lugha maalum ammbazo si kama zile tuzitumiazo katika maisha ya kawaida katika kuwasiliana. Lugha hizi zina herufi na namba ambazo tunazifahamu (A mpaka Z na 0 mpaka 9) ukijumuisha na alama kadhaa kama mkato, nukta, mabano na nyingine nyingi ambazo ni nadra kutumika katika maandishi ya kawaida ya lugha. Mkusanyiko wa herufi na namba hujulikana kama codes na uandikaji wake hufahamika kama coding. Kwa lugha ya kawaida ya kimombo neno codes humaanisha maneno ya siri yasiyoweza kufahamika kwa urahisi na watu wengine isipokuwa wale wachache wenye utaalam maalum waliousomea. Kwa hiyo lugha hizi za kuandikia maelekezo ya kompyuta hufahamika kama programmming languages. Hivyo ni lugha hizi ambazo huifanya kompyuta kujengewa maelekezo ambayo itayatambua na hatimaye kuweza kufanya kazi. Kwa hapa nchini utaalam wa lugha hizi hujifunza katika vyuo mbalimbali nchini kama kile chuo kuku cha Dar es Salaam. Mfano wa lugha hizi za kompyuta ni kama Java, Visual Basic, PHP na C.

Je Kompyuta inayaelewa vipi Maelekezo Haya?

Maelekezo yanayowekwa ndani ya kompyuta hayawezi kuelewekwa moja kwa moja ndani ya sakiti za kompyuta. Yanapaswa kutafsiriwa katika mfumo ambao kompyuta inaweza kuyaelewa. Katikati ya hardware part na software ya kompyuta kuna maelekezo maalum yajulikanayo kama assembler ambayo hufanya kazi ya kutafsiri software part kwenda katika sakiti ya kompyuta. Sakiti ya kompyuta haiwezi kutambua maelekezo yanayokuwa na herufi au namba (ambayo software huundwa) bali hutambua mtiririko wa namba mbili maalum ziandikwazo kama 0 na 1. Kwa hiyo assembler hubadilisha herufi na namba kwenda namba mbili 0 na 1. Kwa mfano neno ‘do’ linaweza kutafsiriwa na assember katika tarakimu 01100 ambazo sakiti ya kompyuta huielewa. Kwa namna hii kompyuta huweza kufanya kazi na kuleta matokeo yanayotarajiwa.

Je Maelekezo au software hutunzwa wapi ndani ya Kompyuta?

Tuliona kuwa kompyuta hutunza kumbukumbu. Na ni uwezo wa kompyuta kutunza kumbukumbu ndiyo unaifanya kuwa chombo cha kipekee katika ulimwengu huu ambacho kinaweza kufananishwa na ubongo wa binadamu na hata kufanya kazi kwa ufanisi. Kumbukumbu za kompyuta hutunzwa katika mfumo wa ki-elektroniki katika kifaa maalum kilicho ndani ya system unit kifahamikacho kama hard disk. Kifaa hiki kina uwezo wa kutunza kumbukumbu kwa muda mrefu na kimeundwa katika mfumo ambao unaruhusu kufuta, kurekebisha na kuandika tena kumbukumbu; kuongeza na kupunguza kumbukumbu. Ni kifaa muhimu katika kompyuta. Huwa kimeunganishwa na motherboard kwa kutumia waya maalum. Kifaa kifahamikacho kama hard disk

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni