Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Februari 19, 2013

TEKNOHAMA - JE UWEZO WA KOMPYUTA HUPIMWA VIPI?


Photo Credity By: http://www.micron.com

 Hakika nguvu ya binadamu katika kufanya kazi hutegemea sana ubongo. Ubongo ndiyo huungoza mwili na ndiyo kama injini ya kila lifanyikalo katika mwili wote. Katika hali sawa na hiyo, kompyuta nayo inategemea kifaa maalum kifahamikacho kama processor au microprocessor. Kifaa hiki ndicho ambacho hufanya kazi zote zinazotakiwa na sehemu nyingine zote za kompyuta. Kifaa hiki pamoja na sehemu ya kutunzia kumbukumbu pindi kompyuta ifanyapo kazi –kumbukumbu za muda; yaani Random accessory memory; ndizo huweza kutanabahisha nguvu ya kompyuta. Na bila shaka umekwisha sikia mtu akisema ‘kompyuta yako ni pentium ngapi’ au ‘kompyuta yako ina RAM kiasi gani’. Hapa anakuwa anazungumzia uwezo wa processor na RAM.

Microprocessor hufanya kazi kwa haraka sana kulingana na jinsi ilivyoundwa. Mpaka leo hii processor ina uwezo wa kufafanua maelekezo (execute instructions) yapatayo bilioni moja kila sekunde, kwa kompyuta aina ya PC. Uwezo huu hupimwa kwa kutumia kiwango kifahamikacho kama Hertz. Microprocessor katika kompyuta aina ya personal za siku hizi zina uwezo wa mpaka 4.0 Gigerhertz (GH).

Nyingi ya processor zinatengenezwa na kampuni ifahamikayo kama INTEL. Kampuni hii huziitza processor zake kwa majina ya Pentium. Na nyingi ya kompyuta aina ya PC hutumia processor za aina hii na ndiyo maana si ajabu ukakuta watu wengi wanafahamu kompyuta kwa kupima kiwango cha ‘pentium’ ilichonacho. Hii ni kwa sababu processor hizi zina matoleo tofauti kuanzia Pentium I, II, III, IV na M na kila moja huwa na nguvu ya juu kuliko ile zilizoitangulia. Kwa hiyo mtu anaposema pentium IV anamaanisha kuwa anataka kompyuta ambayo ni bora zaidi kuliko Pentium I kwani hata muundo wake huonekana tofauti.

Pia katika upande wa utunzaji kumbukumbu kuna kipimo ambacho huitwa megabyte, kwa kifupi MB. Hiki ni kipimo cha utunzaji kumbukumbu ambacho kinaeleza ni kwa kiasi gani maelekezo au data zote zinazotakiwa kusshughulikiwa na zinazotoka kama habari hutunzwa kwa pamoja. Kadiri kipimo hiki kinavyokuwa kikubwa ndivyo kompyuta inakuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa haraka na kwa urahisi zaidi. Kwa kawaida utakutana na kompyuta zenye RAM kiasi cha 256 MB au 512MB na zaidi. Pia kama kompyuta ina processor yenye kiwango cha 2.0 GH au zaidi inakuwa nzuri kea shughuli zote.

Na kwa kawaida kompyuta huuzwa kulingana na viwango hivi viwili, pamoja na kipimo cha tatu ambacho ni utunzaji wa kumbukumbu zisizoweza kupotea (permanent data) katika hard disk. Hii hupimwa kwa kiwango cha Gigabyte (GB). Utakutana na kompyuta aina yenye hard disk kiasi cha 40 GB au 80 GB. Hivyo unaweza kukutana na kompyuta yenye uwezo (specifications) kama ifuatavyo:  

Hard disk 80 GB, RAM 512 MB, Processor speed 2.6 GH Intel Pentium M aina ya Dell.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni