Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Februari 11, 2013

MAANA YA KOMPYUTA


Kompyuta au Kinakilishi katika tafsiri ya Kiswahili ni kifaa au mashine ambayo inafafanua
na kunyumbulisha/kuchakata (process) habari isiyo rasmi (data) kwenda katika habari
rasmi (information) ambayo mtumiaji au mtu anaweza kuielewa na kuifanyia kazi
kutokana na maelekezo kiliyopewa na mtu. Hivyo kompyuta kama kompyuta kwa hakika haifanyi
kazi bila kupewa maelekezo. Bila kupewa maelekezo ifanye jambo gani kompyuta ni kama kopo!
Hii inabadilisha kabisa imani kuwa kompyuta inafanya kazi kuliko binadamu na kwamba ina
uwezo wa juu kuliko hata ubongo wa binadamu! Bila binadamu kompyuta haiwezi kuwapo.
Hiki ni kifaa ambacho hakika kimebadilisha maisha ya binadamu katika karne ya ishirini na
kuweza kuyafanya kuwa rahisi zaidi kwa maana ya kutenda kazi kwa ufanisi wa hali ya juu. Neno
Kompyuta, kwa kimombo ‘Computer’; linataokana na neno ‘computing’ likiwa na maana ya
kukokotoa au kuchanganua hesabu kama kujumlisha, kugawanya, kutoa na kuzidisha. Kompyuta
ina historia ndefu kutoka katika kipindi cha kabla ya kuzaliwa Kristo ambako watu mbalimbali
kama Charles Babbage,

Lakini kifaa cha kwanza kabisa ambacho kinafanana kiutendaji na kompyuta ya leo hii
kiligunduliwa mnamo karne ya 20 (kati ya mwaka 1940 – 1945) ingawa nadharia ya kompyuta na
mashine mbalimbali zinazofanana nayo vilikuwapo kabla kama nilivyosema hapo mwanzo.
Mfululizo wa ugunduzi wa kompyuta ambazo zilikuwa na nguvu ya kutosha kufanya hisabati na
hata kutunza kiasi kidogo cha kumbukumbu ulifanyika kati ya miaka ya 1930 na 1940. Utumiaji
wa vifaa vya ki-eletroniki katika mfumo wa digital ambao uligunduliwa na kuendelezwa kwa kiasi
kikubwa na mtu aliyeitwa Claude Shannon mnamo mwaka 1937 ulifanikisha kwa kiasi kikubwa
kuimarisha ubora wa kompyuta hizo.

Kompyuta inaweza kuelezewa kuwa imepitia hatua kadhaa katika kufikia ubora ilionao sasa. Kati
ya miaka ya 1940 mpaka miaka ya 1950 kompyuta ilikuwa ikitengenezwa kwa teknolojia
iliyojulikana kama vacuum tube. Hii ilikuwa ni teknolojia ambayo ilikuwa ikitumia tubes ndogo
mfano wa vichupa vidogo ambavyo viliondolewa hewa ndani na kuvitengeneza katika mfumo
ambao viliweza kupitisha umeme ambao ndiyo uliunganishwa katika chombo kizima kwa ajili ya
kufanya kazi(kumbuka hata kompyuta ya sasa hufanya kazi kwa kutumia mtiririko wa elektron
ambao umefanywa katika mfumo maalum). Mfano wa kompyuta hizi ni Konrad Zuse's
electromechanical au "Z machines" au Z3 (1941), Atanasoff–Berry Computer (1941), Colossus
computer (1944) ambayo ilitumika kwa ajili ya shughuli za siri katika jeshi la uingereza na
ilitumika katika kupata taarifa za siri za jeshi la ujerumani katika vita ya pili ya dunia, Harvard
Mark I (1944) na kompyuta iliyotumika na jeshi la Wamarekani iliyojulikana kama ENIAC.

Hata hivyo teknolojia hii ya vacuum tubes ilitumika mpaka mwishoni mwa miaka ya 1950 na
mwanzoni mwa miaka ya 1960 kulizinduliwa teknolojia mpya inayofahamika kama transistor
technology. Kompyuta zilizotumia teknolojia hii ziliweza kufanya kazi kwa urahisi zaidi, hazikuwa
aghali sana, zilikuwa ndogo, zilitumia umeme mdogo zaidi na ziliweza kufanya kazi kwa uhakika
zaidi kuliko zile za mwanzo. Kumbuka kuwa kompyuta za mwanzo zilikuwa na ukubwa sawa na
chumba kikubwa cha nyumba! Teknolojia ambayo mpaka sasa inatumika katika utengenezaji wa
kompyuta inaitwa integrated circuit technology. Teknolojia hii ilizinduliwa mnamo miaka ya 1970.
Ni teknolojia hii ambayo imesababisha kuzaliwa kwa kompyuta ambazo ni ndogo zaidi kuweza hata kubebwa katika kiganja cha mkono! Hii ni kea sababu ya kuundwa kwa kifaa kijulikanacho
kama microprocessor ambacho ndicho kama ubongo wa kompyuta. Kifaa hiki kina ukubwa wa
kama saizi ya milimita tano kwa nne. Ingawa kina umbo ndogo sana lakini kina jumla ya zaidi ya
transistor (sakiti ndogondogo zinazofanya kazi kwa ushirikiano) milioni moja!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni