Mtayarishaji

Morning Star Radio

Alhamisi, Februari 14, 2013

LICHA YA KUWAPO AINA KUU NNE; KOMPYUTA ZIMEUNDWA KATIKA MSINGI MMOJA!


Licha ya kuwa na aina za kompyuta lakini bado kuna msingi ambao zote huutegemea. Msingi huo ni kuwa na sehemu kuu mbili; sehemu kuu ya kutengeneza habari kutokana na data zilizoingizwa ijulikanayo kama Central Processing Unit au CPU kwa kifupi na sehemu ya kuingizia data na kutolea habari iliyokwisha tengenezwa kwa ajili ya faida ya mtumiaji ijulikanayo kama peripheral devices. Kwa hiyo data huingizwa kupitia sehemu zinazofahamika Kama peripheral devices na kupelekwa ndani ya CPU ambako hunyumbulishwa na kufafanunuliwa na hatimaye kutoa kile kilichokusudiwa kupitia tena peripheral devices hizohizo. CPU hufanya kazi ya kufafanua data (processing) kulingana na maelekezo ya mtumiaji. Tuone sehemu mbalimbali za kompyuta ambazo huifanya kazi ya kompyuta kutekelezeka kwa ufanisi.



Ubongo wa Kompyuta (Central Processing Unit)



Hii ni sehemu maalum kabisa katika kompyuta. Ndiko ambako maamuzi yote kuhusu data na habari hufanywa ili kuhakikisha kuwa mambo yanakwenda vyema. Ni kama ubongo wa binadamu ambao huamua mambo yote yanayohusiana na shughuli zote za mwili ili kumfanya aishi katika afya njema. Sehemu hii ya kompyuta huwa ndani ya kifaa kiitwacho computer case ambacho kinafunika ‘ubongo’ huu wa kompyuta. 

Computer Case inaweza kuwa bapa na yenye umbo la msitatili au mraba (kwa aina ya personal computers) ambayo huwekwa katika meza ili iweze kutumika vyema. Aina hii ya computer case inajulikana kama desktop case na ndiyo maana kompyuta huitwa desktop computer. Pia computer case inaweza kuwa na umbo lililosimama, kama umbo la mche msitatili na lijulikanalo kama Tower case – na ndiyo huzaa jina la Tower computer. Lakini kwa notebook computer na palmtop computers computer case huwa imunganishwa na sehemu ya peripheral kiasi kwamba ni vigumu kuweza kuifafanua vyema.



Ubongo wa kompyuta huwa ni muunganiko wa sehemu mbalimbali ambazo kwa pamoja huwekwa katika mfumo mmoja ujulikanao kama motherboard. Muundo wa motherboard hutofautiana kutegemeana na aina ya kompyuta (mtengenezaji) na ukubwa wa kompyuta yenyewe na hata toleo (version) la kompyuta husika. Kompyuta aina ya desktop ina motherboard tofauti na kompyuta aina ya notebook. Pia kompyuta toleo la mwaka 1995 ina muundo wa motherboard ulio tofauti na lile la toleo la mwaka 2005.



Ubongo wa kompyuta (CPU) huwa na vifaa muhimu vifuatavyo:



Kifaa ambacho ni mkusanyiko wa mamilioni ya sakiti ndogondogo zijulikanazo kama transistors. Sakiti hizi zinakwa na ukubwa wa chini ya unywele mmoja wa nywele za binadamu! Kifaa hiki ndicho ambacho kinachukuliwa kama moyo au ‘roho’ ya kompyuta. Bila kifaa hiki kompyuta haiwezi kufanya lolote. Kifaa hiki kinajulikana kwa jina la microprocessor. Ni kifaa hiki ambacho hupokea mamilioni ya maelekezo kutoka kwa mtumiaji na kuyafanyia kazi ili kutoa majibu yanayotakiwa. Kina uwezo wa kufafanua na kunyumbulisha data kwa uwezo wa hata kufikia maelekezo trilioni moja kwa sekunde! (hii ni kulingana na ukubwa na uwezo wa microprocessor hiyo kutegemeana na aina ya kompyuta).



Kifaa kingine muhimu ni kitunza kumbukumbu kijulikanacho kama random access memory chip ambacho hutunza kumbukumbu zinazofanyiwa kazi na kompyuta. Kumbukumbu hizi huhifadhiwa katika mfumo ambao ni wa muda tu; ikiwa na maana kwamba mfumo huu hupoteza kumbukumbu hizo mara tu umeme ambao unaozunguka katika sakiti nzima ya kompyuta unapotoweka. Kifaa kijulikanacho kama random acess memory



Kifaa kingine ni mkusanyiko wa nyanya ndondogo sana ambazo huunganishwa pamoja na kufungwa vyema ndani ya material aina ya plastiki. Kifaa hiki hupitisha data ndani na nje ya motherboard. Ni kama barabara ambayo inaunganisha mji mkubwa ili kufanya mawasiliano kuwapo baina ya watu. Kifaa hiki kinafahamika kama system bus.


System bus (utepe manjano)



Pia kuna vifaa mbalimbali ambavyo vinahusika na utoaji wa sauti, picha na kadhalika. Pia matundu ya aina mbalimbali ambayo huwezesha uunganishwaji wa sehemu za nje ya motherboard yaani peripheral devices.



Sehemu Za Nje ya Motherboard (Peripheral Devices)



Hizi ni sehemu ambazo zinakamilisha ufanyaji kazi wa kompyuta. Sehemu hizi ziko nje ya system case na zinakuwepo katika kompyuta kulingana na matumizi ya mtu husika ingawa kuna sehemu ambazo lazima ziwepo (basic peripheral devices). Sehemu hizi za kompyuta hujulikana pia kama sehemu za kutoa na kuingizia habari na data au kwa jina la kitaalam kama input and output devices. Sehemu hizi ni kama zifuatazo:



Sehemu ya kuingizia maneno na maelekezo maalum ijulikanayo kama keyboard. Hiki ni kifaa ambaco kina mkusanyiko wa herufi (A mpaka Z) na namba 0 mpaka 9. Kifaa hiki kina mkusanyiko wa vitufe au buttons ambazo herufi au namba hizo huandikwa. Mtumiaji wa keyboard anapaswa kubonyeza (press) vitufe hivyo ili kuweza kuingiza malekezo haya (herufi na namba) katika kompyuta. Pia keyboard huwa na buttons maalum ambazo huingiza malekezo maalum kea ajili ya ufanisi wa kazi wa kompyuta. Tutazungumzia zaidi sehemu hii.



Sehemu ya kukuwezesha kuona nini unakifanya katika kompyuta. Huwezi kwenda kwa mfano sokoni ilihali hauoni. Unahitaji kuona barabara na kufahamu soko lipo wapi ili uweze kufika kwa urahisi. Vivyo hivyo unapokuwa unatumia kompyuta au unafanya kazi na kompyuta unahitaji kuona kile unachokifanya. Unahitaji kusikia kile unachokitarajia. Sehemu hii ya kompyuta hujulikana kama monitor. Monitor ina umbo kama la runinga ambayo umezoea kuiona na kwa uhalisia teknolojia ya uundwaji wake ipo sawa na ya runinga isipokuwa marekebisho kidogo. Monitor ndipo mahala pekee pa kuweza kufahamu nini kinaendelea ndani ya kompyuta kwani shughuli zote za utengenezwaji na utoji habari huonekana katika kifaa hiki.



Sehemu ya kuweza kuingiliana na monitor na kufanya kile unachikihitaji na ambayo hufanya kazi kwa kushirikiana na keyboard ni sehemu ya tatu katika hili kundi la peripheral devices. Sehemu hii inajulikana sana kama mouse. Mouse ni kifaa ambacho mtumiaji hukitumia kuwasiliana na kompyuta (CPU) ili kuzaa au kutoa kile kinachotarajiwa. Kifaa hiki huwa na mahali ambapo unabonyeza kwa kutumia kidole na ubonyezawji wa kidole hiki husafirisha habari katika kompyuta na kuilekeza ifanye nini. Mouse huonekana katika kompyuta kama mshale na mshale huu hutembea katika monitor kumuwezesha mtumiaji kuamua nini cha kufanya. Mshale huu hujulikana kama cursor kwa kimombo.



Sehemu hizi tatu za kwanza katika kundi la peripheral devices zinategemeana na hujulikana kama basic input & output devices. Hii ina maana kwamba sehemu hizi ni lazima ziwepo ili kuifanya kompyuta ifanye kazi zilizo za muhimu. Sehemu nyingine muhimu ni zile zinazotoa na kuingiza sauti. Sehemu hizi hufahamika kama input

and output sound devices. Mfano wa sehemu hizi ni kama speakers, microphones, webcam, cameras na nyingine nyingi. Pia sehemu za kuingizia picha na kutolea picha kama cameras. Aina mbalimbali za Microphones



Sehemu nyingine muhimu ambayo ni ya muhimu sana inajulikana kama printer. Ni kifaa ambacho hutumika katika kuchapa matokeo ya ufafanuzi wa kompyuta ulio katika mfumo wa maandishi (text) kwa shughuli mbalimbali anazozihitaji mtumiaji. Kifaa hiki kina uwezo wa kutoa maandishi na picha zilizo na zisizo na rangi. Kifaa hiki kinatofautiana katika utengenezwaji kulingana na mahitaji ya watumiaji.



Sehumu tulizozizungumzia hapo juu ndizo sehemu zinazojumuisha peripheral devices. Kwa hakika sehemu hizi ni muhimu katika kuifanya kompyuta iitwe kompyuta kwani ndizo zinazowezesha kupata matokeo ambayo binadamu anayahitaji katika maisha yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni